IMETIMIA Msemaji wa Yanga Jerry Muro Afungukiwa na TFF Kujihusisha na Maswala ya Soko

Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imetangaza kumfungia Jerry Muro kupitia ile kesi yake kwamba amekuwa akiipinga na kuishambulia TFF kwenye vyombo vya habari.

Mkuu huyo wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Yanga, Jerry Muro amefungiwa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka.

Kikao cha Kamati ya Maadili ya TFF, kilikaa bila ya Muro kuwepo kwa kuwa wakati mwaliko unatoka alikuwa nje ya Dar es Salaam.

Katika makosa matatu aliyoshitakiwa, moja amekumbana na adhabu hiyo, moja amepigwa faini ya Sh milioni 3 na moja ameonekana hana hatia.

Muro ambaye yupo mapumzikoni Machame mkoani Kilimanjaro ambako ni kwao.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. MMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMMhhh

    ReplyDelete
  2. MSEMA KWELI MARA ZOTE HUWA HAPENDWI. JERRY KILA WAKATI ANAPEWA ADHABU KWA SABABU YA KUSEMA UKWELI. LAKINI MSEMA KWELI DAIMA NI MPENZI WA MUNGU. SAWA TU.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad