Mashabiki wa Wema Sepetu waushangilia uamuzi huu wa Diamond

Hakuna kitu ambacho mashabiki wa Wema Sepetu wanakipenda kama kuona kuwa kuna amani kati yake na Diamond.

Pamoja na kuwepo kwa tension kubwa kati ya wawili hao licha ya kila mmoja kuwa na hamsini zake sasa – yaani Diamond kuhamishia mabaha yake kwa Zari waliyejaaliwa mtoto wa kike, Tiffah na Wema kuwa mikononi mwa staa mwenzake, Idris Sultan, mambo yanaonekana kuanza kunyooka.
Jumanne hii Diamond aliwafurahisha sana mashabiki wa Wema pale alipoipromote show ya Black Tie iliyoandaliwa na Wema na Idris, July 9.

Ikumbukwe kuwa wiki kama tatu zilizopita Wema alisikika kwenye mahojiano akimtupia lawama ex wake huyo kuwa alimfanyia fitina asiupate ukumbi kwa King Solomon kwaajili ya show yake hiyo ambapo Christian Bella atatumbuiza.
Kwa hatua hiyo huenda wawili hao wameamua kuyaacha yapite na wagange yajayo.

Post ya Diamond kuhusu show hiyo tayari imevunja rekodi kwa kuvutia comments nyingi zaidi. Hadi sasa zimefika takriban 5,000! Comments nyingi zinampongeza kwa uamuzi huo.
Naye Wema amepost picha mbili zilizokatwa na kuziacha kuanzia kidevuni kuja chini ambazo zinaonekana wazi kuwa ni picha za Diamond. Wakati wengi wakifurahia,upande mmoja lakini haujakipokea kikombe hicho cha chai – Team Zari!

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. mimi na familia yangu tumefurahi sana.

    ReplyDelete
  2. Nasemajeee ngoma inogileeeee watu wanarudiana hawa...haahaah true love never dies....mbona zari anampostig ivandon si wana amani wakat mpambe wa ivan anamponda zari na d...lakn aman si ipo btn zari n her x...na d wala halalamikii basi acheni na wema awee na aman na d...ama nenenene....hahahahhaaa movie ipo patamuuuu mnoo

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad