KIMENUKA:Waliotafuna Fedha za Mikopo Wapewa Siku Saba Kuzirejesha

Wafanyakazi wa Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vikuu (HELSB)na wa vyuo vilivyohusika kufanikisha malipo ya fedha za mikopo kwa wanafunzi hewa kuchukuliwa hatua kali za kisheria pamoja na kurudisha fedha zilizochukuliwa na wanafunzi hao.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mh. Joyce Ndalichako .

“Kutokana na mambo yaliyobainika serikali imechukua hatua ikiwemo kuvitaka vyuo vikuu vilivyopokea fedha za wanafunzi ambao hawapo chuoni vinatakiwa virejeshe fedha hizo ndani ya siku Saba kuanzia leo, ” amesema.

Amesema vyuo vinatakiwa kuweka mfumo mzuri wa kuhifadhi kumbukumbu za wanafunzi kuanzia usajili, matokeo ya majaribio na ya mitihani na namba za akaunti za benki ambazo fedha za mikopo hulipwa ili kuondoa udanganyifu.

“Bodi ya mikopo inapaswa kuchambua na kuingiza mara moja mabadiliko ya taarifa zote za wanafunzi kama zilivyopokelewa kutoka vyuoni ili kuepusha ulipaji wa fedha kwa wanafunzi wasiostahili,” amesema
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. NDIO ZIRUDISHWE HARAKA SANA

    ReplyDelete
  2. Huu ndio uadilifu tunao utaka na kuuona.. Ujanja Ujanja hatuupendi... Kula kimisheni town kusitishwe tuna taka nguvu jasho. Unakula kwa kazi yako na si ki hewa Hewa.. Baba Magu na sisi wote tunalikataa hilo!! Hongera mama Ndalichako Kazi yako ni Nzuri na Tunaipenda... Tena warudishe haraka Sana

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad