Madada wa The Kardashians Wakanusha Kauli ya The Game Kuwa ‘Alipita’ na 3 Kati yao

Madada wa The Kardashians wanadai kuwa rapper The Game anadanganya anaposema kuwa amewahi kulala na watatu kati yao kwenye wimbo wake mpya, Sauce.

Kwa mujibu wa TMZ, Game alipita na mmoja tu. Vyanzo vilivyo karibu na familia hiyo maarufu, imewaondoa Kylie, Kendall, Khloe, Kourtney na Kris kwenye orodha hiyo na kwamba hakuna kati yao aliyekula uroda na Game.

Vyanzo hivyo vimekubali kuwa mke wa Kanye West, Kim Kardashian ndiye aliyewahi kuwa na uhusiano na Game miaka ya nyuma. Khloe na Game wamekuwa marafiki kwa muda, lakini vyanzo hivyo vimesema haukuwa uhusiano zaidi ya ule wa kawaida.

Inasemekana kuwa Game alimfuata Kanye kuomba ruhusa ya kuutoa wimbo huo na Yeezy alitoa baraka zake. Hata hivyo, Game anashikilia msimamo wake kuwa alipita na watatu kati yao.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad