Malaika Afungukia Alivyoingizwa Mjini China

MSANII wa Bongo Fleva, Malaika Exervery amesema katika vitu ambavyo haviwezi kutoweka kichwani mwake ni pamoja na kutapeliwa wakati alipoingia nchini China kwa mara ya kwanza kwenye Jiji la Hong Kong.


Akizunguza na Juma3tata, Malaika anasema kuwa tukio la yeye kuingizwa mjini lilitokea mara baada ya yeye kuwekwa kuzuizini kwenye uwanja wa ndege kwa saa 16 akihisiwa kuwa amebeba madawa ya kulevya.

“Nilinyang’anywa mizigo yangu yote hadi simu, nilikaa pale kwa muda mrefu mpaka naachiwa usiku ulikuwa tayari umeingia na nilirudishiwa simu tu bila laini kwahiyo ikabidi nianze kutafuta duka ili ninunue laini niwasiliane na mwenyeji wangu,” anasema.

Akaongeza: “Bahati nzuri akatokea Mchina mmoja ambaye alikuwa akiuza laini. Kwasababu nilikuwa na umuhimu nayo kwa haraka, nilinunua bila kuuliza mara mbili. Nikafanya mawasiliano na mwenyeji wangu, kisha nikaondoka.

“Lakini baadaye nilipokuja kufuatilia nikagundua kuwa ameniuzia kwa bei ya juu sana. Yaani sikuwa na hamu. Kweli mjini usipokuwa mjanja unapigwa.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad