Mapacha Waliofanyiwa Upasuaji Kupasuliwa Tena


Madaktari bingwa nchini wakisaidiana na wataalamu kutoka Misri, wanajipanga kuwafanyia upasuaji watoto pacha waliotenganishwa, Eliud na Elikana Mwakyusa (3) wakazi wa Kasumulu, Kyela mkoani Mbeya.

Katika upasuaji waliofanyiwa awali, waliwekewa njia za dharura na muda mfupi za haja ndogo na kubwa, hivyo wanafanyiwa upasuaji mwingine kuwekewa njia za kudumu.

Ofisa Habari wa MNH, John Stephen amesema upasuaji wa pacha hao umefuatia baada ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) kuanza upasuaji kwa watoto wanane, wenye matatizo ya njia ya mkojo na mfumo wa hewa na chakula.

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad