Mbwana Samatta Aipeleka Timu ya Genk Hatua Nyingine Ligi ya Europa League

Mtanzania mshambuliaji wa Kimataifa, Mbwana Ally Samatta amepata nafasi ya kucheza hatua ya makundi ligi ndogo ya klabu Ulaya, Europa League.

Hii ni baada ya klabu yake ya KRC Genk ya Ubelgiji kupata ushindi wa jumla ya mabao 4-2 dhidi ya wapinzani wao Lokomotiva Zagreb ya Croatia.

Genk walipata ushindi wa 2-0 mechi iliyochezwa jana jioni.

Klabu hizo mbili zilitoka sare 2-2 mechi ya mkondo wa kwanza.

Samatta alifungia klabu yake bao la kwanza dakika ya pili naye mwenzake Leon Bailey akafunga la pili muda mfupi baada ya mapumziko.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad