Ridhiwani Kikwete Awapongeza AliKiba na Diamond ‘Mmeonyesha Umuhimu wa Kuwa Mastaa’

Mbunge wa Chalinze Mhe. Ridhawani Kikwete amewapongeza wasanii wa muziki, Diamond Platnumz na AliKiba kwa kutoa msaada wa tsh 41milioni kwa ‘GSM Foundation’ ili kusaidia jitihada za taasisi hiyo za upasuaji wa watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi.
Diamond na Ali Kiba

Mtoto huyo wa Rais mtaafu, amewapongeza wasanii hao kwa kuonyesha kuguswa na kusaidia matatizo ambayo yanatokea katika jamii.

“Katika vitu vimeonyesha umuhimu wa kuwa stars katika jamii yetu ni hili mlilolifanya wadogo zangu. Ni jambo la kusifiwa na Mungu atawalipa kwa kuwaongezea maarifa ya kufanya kazi zenu vizuri,” Ridhiwani aliandika katika instagram yake.

Aliongeza, “Pia niwapongeze sana GSM Foundation kwa kazi nzuri mnayoifanya. Kutoa si utajiri, ni moyo na mungu atakuzidishia ndugu mkurugenzi Gharib pale ulipotoa. Kila la kheri katika kusaidia jamii yetu yenye mahitaji. Peace to you,”

Siku chache zilizopita Diamond Platnumz alitoa msaada kwa taasisi hiyo wa tsh 20 Milioni na baadae AliKiba na yeye aliamua kutoa tsh 21 Milioni.

Bongo5
Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Lazima awasifie
    Punda wake

    ReplyDelete
  2. Juu. Ndiyo mfano WA kuigwa Na social responsility..back to the society..na MO ameshatoa ngapi Na Wema? manake Mzee Majuto hata hosp Na gari la kupeleka wagonjwa vyote bure anafanya.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad