Taarifa kuhusu uteuzi wa Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Uliofanywa na Rais Magufuli Leo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Agosti, 2016 amemteua Bw. Andrew Wilson Massawe kuwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Kabla ya uteuzi huo Bw. Andrew Wilson Massawe alikuwa Mkurugenzi wa Mifumo ya Kompyuta katika Benki Kuu Tanzania (BOT).

Bw. Andrew Wilson Massawe anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dkt. Modestus Francis Kipilimba ambaye ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.

Uteuzi wa Bw. Andrew Wilson Massawe unaanza mara moja.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
25 Agosti, 2016
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Asante kwa taarifa.Ila daah,Baba kabana koo jamani.
    Yaani watu wameuza magari,wengine wameyaacha tu hasa wale wenye magari 3,4 kwenye familia moja sasa wameamua kutembelea gari moja badala ya kila mtu na gari lake,kisa mafuta,uwiiiiiiiiiii tunaisoma wote kwa kweli.HESHIMAAAAAAAAAAAAAAAA.CHEZEA HAPA KAZI TU.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad