Uchaguzi Mkuu wa 2015 Ulikuwa Mgumu Sana Kwa CCM - Mangula

Kauli hiyo imetolewa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho upande wa Bara Philip Mangula wakati akizindua Daftari la Mashina ya chama hicho ambayo ndiyo chimbuko la wanachama wake kwa lengo la kuimarisha chama hicho na kuongeza wanachama.

Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika katika kijiji cha Utiga kata na halmashauli ya Wang'ing'ombe mkoani Njombe Mangula amesema kuwa uchaguzi huo ulikuwa wa tofauti na miaka mingine ingawa kwa sasa ukirudiwa utakuwa rahisi.
Katika wilaya ya Wang'ing'ombe chama hicho kinadai wa kuongoza kuwa na wanachama wengi na kupata madiwani wote wa CCM na kuwa sasa kinazindua kitabu hicho ili kuimarika zaidi.

Kitabu hicho kinazinduliwa pamoja na shina la chama hicho huku vitabu hivyo vikigawiwa kwa mabarozi 125 na viongozi wa kata 24 na wanachama lukuki wakijiunga na chama hicho na kukabidhiwa kadi za chama hicho na Mangula.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad