Afikishwa Mahakamani Kwa Kumuita Rais Magufuli ni Kilaza

ELIZABETH Asenga (40), mkazi wa jijini Dar es Salaam amepandishwa kortini jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kuandika maneno ya kumkashifu Rais John Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa What’s App.

Akisomewa mashtaka yake na Leonard Chalu, wakili wa serikali, mbele ya Hakimu Huruma Shahidi, mwanamama huyo, alidaiwa kufanya kitendo hicho kilicho kinyume na Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.

Wakili Chalu alidai kuwa, mnamo tarehe 06 Agosti mwaka huu, mtuhumiwa huyo aliandika kwenye mtandao wa what’s App ujumbe uliosomeka;

“….Rais kilaza kama huyu wetu, angalia anampa Lissu umashaghuli… f****l** lile, kwanza picha yake ukiweka ofisini ni nuksi tupu na ukiamka asubuhi ukakutana na picha yake, siku yako inakuwa ina mkosi mwanzo mwisho.”

Hata hivyo, mshitakiwa Elizabeth, alikana mashtaka hayo huku wakili wa serikali akidai kuwa, upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Mtuhumiwa alipewa dhamana yenye masharti yanayohitaji wadhamini wawili huku kila mmoja akitakiwa kusaini hati ya shilingi 3 millioni.

Kesi hiyo imeahirishwa na inatarajia kutajwa tena mnamo tarehe 22 Septemba, mwaka huu.

Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. akome
    mama zima hovyoo

    ReplyDelete
  2. Awamu watafungwa wengi
    Ongezi magereza
    Tanzania ya Leo Kama Enzi ya Hitler

    ReplyDelete
    Replies
    1. Inaonekana huo uhitler unao nyumbani kwenu maana wazazi wako walivyokulea kikatili mpaka akili zikakuruka Awamu hii haina uhitler ila inairudisha nchi ktkt mstari uliopotea na hata wewe kichaa utanyooka tuu kwa awamu hii bila hata ya kwenda magereza

      Delete
    2. Koma wewe na mama yako asiyejuwa Nani Kampa mimba yako
      Atanyoka mama yako na wewe kila kukicha kuranda bungeni mpk ukazaliwa wewe
      pumbavu wewe

      Delete
  3. Mmmmh hatari sana hii...

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad