Majibu ya Mkurugenzi NHC Kuhusu Kudaiwa Kuingiza Siasa Kwenye Shirika Hilo

Baada ya Shirika La Nyumba la Taifa kupitia kampuni ya udalali kutoa samani mbalimbali katika jengo la Club Bilicanas na jengo lenye Ofisi ya Free Media kufuatia mmiliki wa ofisi hizo Freeman Mbowe kudaiwa kutolipa deni ambalo ilielezwa kuwa anadaiwa na shirika hilo.

Aidha hivi karibuni ziliripotiwa habari kuwa Mbowe amesema kinachofanyika ni siasa kwani wanafanya kama kumkomoa kwa sababu mara zote amekuwa mstari wa mbele kuikosoa serikali kuhusu hali ya siasa nchini.

Kupitia kipindi cha funguka kinachorushwa na kituo cha television cha Azam Tv, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu amejibu madai hayo kwa kusema……..

’National Housing ninayoiongoza mimi haijawahi kusukumwa kwa mkono wa siasa, na tungekuwa tumesukumwa na mkono wa siasa tusingefanya haya tuliyoyafanya kwa muda mfupi, taasisi za serikali zimeshagusa machungu yetu, hata chama tawala idara yake makao makuu‘

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Mbona NHC wametugusa wengi?Tatizo ni kwamba Mbowe ni mwanasiasa ndio maana jambo hili kwake limekuwa kubwa na kuchukuliwa hivyo,
    ukweli hata yeye Mbowe anaujua kwamba anadaiwa kisheria,Longolongo haisaidii,ukiwa kama kiongozi dawa ni kulipa deni ili kuepuka kashfa ya kuwa kiongozi bora.

    ReplyDelete
  2. Inazidi kunitia wasa wasi, Ikiwa Pango anatuibia hivi. Je KODI HUKO TRA AMESALIMIKA HUYU!!!!!!!! Naomba arudishwe katika uaminifu kabla hatujafikia ukingoni mwa ukuta. Mwisho ni madongo polomoka... TRA Kazi mnayo na kurudia ulipaji halali na mapitio ni Wajibu wenu na lengo ni ukusanyaji halali. MAGUMASHI NA DILI... HATUZITAKI NA TUMELIKATAA HILO. Wachapa kazi ingieni Kazini.. Hapa Kazi Tu

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad