Msigwa 'Awatolea Uvivu' Mawaziri wa Magufuli!

Alichangia mswaada wa haki ya kupata taarifa mbunge wa Iringa mjini Mch Piter Msigwa amesema taifa limesinyaa kwa sababu mawaziri ni waoga wa kumkosoa hata kumshauri rais. " Huu mswaada mbovu ulipita kwenye baraza la mawaziri kwa sababu mnaogopa kumkosoa rais, huyu amekuwa kila kitu na kufungia kila kitu". Aliongeza "Mkileta mswaada kama huu sisi hatuogopigi kumkosoa, ukienda maabara ukaambiwa unaendesha haufungi maabara bali unatafuta tiba".


"Sasa ninyi mmekuwa waoga mpaka mnatia huruma, na rais wenu hana urafiki atawafurumua huko mje huku back bencher kukutana na sheria mbovu mlizopitisha wenyewe, hamuoni wenzenu mliokuwa nao tumekaa nao huku?" alisema. Amesema anashamshangaa Dr Mwakyembe na usomi wake kutumwa kupotosha sheria ya vyama vya siasa. Hivi wewe Mwakyembe na usomi wako kweli ile ndiyo tafsiri ya sheria ya vyama vya siasa? Kweli? "Eti kuna watu mnachangia eti mnalinganisha Tanzania na nchi za Ulaya kwa demokrasia, sisi tulinganishe na Rwanda"

Amewataka wabunge wa Ccm kuacha kuamini watatawala milele kwani hata Roma Empire ilianguka. "Hata Lowassa alikuwa huko kwenu, leo tunapigwa naye, tunafungwa naye na maji ya washa washa tunamwagiwa naye"
Tags

Post a Comment

4 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Replies
    1. Msigwa!! hapa umekwenda mbali Kijana. Tafsri na Upeo wa fikra zako ulizo tuletea zote ni Potofu kiasi ambacho umejaribu kujiweka kando na kuweza kumnasibisha Rais wa Jamuhuri ya muungano kuwa ni Rais Wenu ( Je sisi ni mob au syndicate of wrong doers/ Violators) Jirekebishe na ujue kuitumia Lugha ipasavyo na Mahali pake. Uliyo zungumza yote hayana mantiki wala Maudhui .. Saidi ya kutaka kutuonesha unajaribu kujitutumua kama puto au pulizo ukija mwiba unanyea. Chunga ulimi Dogo!!

      Delete
  2. asante MCHUNGAJI kutokuwa mnafiki.Na maandiko yanatufundisha..if you want to know the truth..you should go beyond your palace as people in your palace will give you want YOU WANT TO HEAR...NOT the TRUTH..

    ReplyDelete
  3. Kumbe mlimchukua Lowassa ili mumtoleee mfano duh kwa kweli binadamu ni watu hatari sana.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad