Bangi Yawatokea Askari 10 Puani..Watiwa Mbaroni

 Jeshi la Polisi limetikiswa baada ya maofisa wake 10 kutiwa mbaroni wilayani Siha mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kuwaachia watuhumiwa wa shehena ya bangi.

Tukio hilo ambalo limekuwa gumzo, lilitokea Jumanne iliyopita kwenye Kijiji cha Olmolok baada ya maofisa hao kudaiwa kukamata magunia manane yaliyosheheni bangi yakisafirishwa kwenda nchini Kenya.

Ofisa Mnadhimu wa jeshi hilo Mkoa wa Kilimanjaro, Koka Moita kwa niaba ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, alithibitisha kuwapo kwa tukio hilo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad