Harufu Soko la Samaki Feri Imekuwa Kero..Wateja Wakimbia

Mkuu wa Wilaya ya Ilala,Sophia Mjema amesema harufu mbaya inayotoka kwenye soko la samaki la feri inasababisha baadhi ya wateja wasifike sokoni hapo kununua samaki.

Akikabidhi bodi mpya ya soko hilo, Mjema amesema wateja wasipofika kununua samaki mapato ya soko yanapungua na kusababisha soko liendelee kuchakaa.

Ameipa bodi mpya ya soko hilo miezi mitano kumaliza tatizo la harufu hiyo na kuongeza mapato vinginevyo ataivunja.Mkuu wa wilaya alielezwa na Meneja wa Soko, Nico Eliakimu kuwa wanakusanya ushuru wa Sh 105 milioni kwa mwezi

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad