Majibu ya Amber Lulu Baada ya Kudaiwa Alikamatwa na Madawa ya Kulevya

Leo mtangazaji Soudy Brown amepiga story na  Amber Lulu, mwanadada maarufu kwenye mtandao wa Instagram ambaye inaelezwa kuwa aliwahi  kutoka kimapenzi na Rapa Young Dee. Sasa wiki iliyopita kupitia U Heard ilitoka stori kwamba Amber Lulu amekamatwa na madawa ya kulevya akiwa uwanja wa ndege.

Soudy Brown amempata Amber Lulu kwenye line na ameeleza kuwa sio kweli kuwa alikamatwa na madawa ya kulevya kama inavyodaiwa na hajawahi kujihusisha na ishu za aina hiyo isipokua wakati anadate na Young Dee ndio stori za kutumia madawa ya kulevya zilianza kuzagaa mtaani.

Watu wanasema mimi nilikamatwa sijui sipatikani kitu ambacho sio kweli, mi nilikwa Arusha na sikuaga mtu kwasababu ni maisha yangu na hua sina utaratibu huo, na huyo Gigy Money aache maisha yangu afanye mambo yake, mimi nimetoka Arusha kuja Dar kutafuta maisha.  kwetu Kurasini hapo, Mimi Passport yangu ilisumbua na sio kukamatwa na madawa ya kulevya:- Amber Lulu

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad