Barakah The Prince aumizwa na mengi kwenye muziki

Hitmaker wa Nisamehe, Barakah The Prince ametoa yake ya moyoni kuhusu kinachomuumiza kwenye Bongo Fleva.

Muimbaji huyo amedai uteam ndio sababu iliyochangia kukosa tuzo kubwa za kimataifa za muziki. Kauli hiyo ya muimbaji huyo imekuja wakati ambapo kumekuwa na vita ya maneno ya kejeli na matusi kati ya Ommy Dimpoz na Diamond Platnumz.

Kupitia mtandao wa Instagram, Barakah ameandika:

Mungu saidia game ya #Tanzania tupendane na tuheshimiane(….)inasikitisha sana team team zinarudisha sana music industry yetu nyuma..tumekosa tunzo nyingi kubwa na zamaana,sababu ya kukosa umoja na mshikamano wa mashabiki..tunatengeza matabaka baina ya mashabiki na mashabiki…Heee Mwenyezi MUNGU ingilia kati swala hili.. #NISAMEHE link kwa bio yangu

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad