HEKAHEKA: Majibu ya Cheki Budi Kuhusu Mtoto Anayedaiwa ni Wake

Leo November 15 2016 Heka Heka ya Leo Tena ndani ya Clouds FM imefanya muendelezo wa hekaheka ya jana iliyohusu mtoto ambaye alifika katika Studio za Clouds FM siku ya Ijumaa November 11 2016 na kukutana na Geah Habibu akiomba kukutanishwa na baba yake mzazi ambaye ni msanii wa Bongo Movie aitwaye Cheki Budi.

Heka Heka ilizungumza na mama mzazi wa wa binti huyo ambaye ameeleza kuwa alikuja Dar es salaam kwa mara ya kwanza mwaka 2005 akiwa ni mke wa mtu na alikaa kwa siku 9 tu na wakati akikaribia kuondoka alienda Club ambako alikutana na mwanaume ambaye anatajwa kuwa ni Cheki Budi ambaye muigizaji wa Bongo Movie na ni siku hiyo hiyo alipata ujauzito.

Sasa Leo Geah Habib amempata Cheki Budi kazungumzia kuhusu yeye kudaiwa kuwa yule ni mtoto wake, Cheki Budi amesema……
’Nipo tayari kuonana naye, ikiwa maelezo hayajanitosheleza nitapima DNA  kama mtoto ni wa kwangu mimi nitampokea, hivi kweli mimi nitakumbuka miaka 11 iliyopita halafu mtu mwenyewe anasema ametembea na mimi siku moja’

Kusikiliza Full Stori, Bonyeza Play Hapa chini:

Post a Comment

5 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Nimekupendaje Chekibudi,safi sana.

    ReplyDelete
  2. Ukimwi,ukimwi,unachukua mtu club unaenda nae nyumbani,halafu una....bila kinga,uwiiiiiii!

    ReplyDelete
  3. Chekibudi KIWEMBE

    ReplyDelete
  4. Mwanaoooooooooooooooooooooooooooooooooooo,bila hata DNA.
    MNAFANANA MBAYA

    ReplyDelete
  5. Hatakama sio mwanao, hilo ni 'EMBE DODO' chini ya mwarobaini, kalelewa tangu mtoto mpaka amekuwa mkubwa, hujachangia hata senti moja, bado unaleta longo-longo za DNA. Mimi ni mweusi tii, laiti kama ningekuwa naweupe angalau kidogo tu, huyo mtoto ningemchukua!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad