Kamanda Sirro Afunguka Kuhusu Wasiwasi wa Makonda kwa Jeshi la Polisi

Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuonekana kuwa na shaka juu ya jeshi la polisi kwenye harakati za kutokomeza matumizi ya Shisha – Kamanda wa Polisi mkoa wa Dar es salaam Simon Sirro amefunguka juu ya tuhuma hizo.

Kamanda huyo amekiambia kipindi cha Sun Rise cha Times FM leo kuwa jeshi la polisi wanafanya kazi kwa mujibu wa Sheria na Operesheni ya kutokomeza Shisha jijini inaendelea kama kawaida kilicho baki ni mwanasheria mkuu wa serikali kuandaa mashtaka kwa watuhumiwa.

“Watu wamekamatwa ni wengi, kimsingi kazi inafanyika, sasa huo ni wasiwasi kama wasiwasi basi unabaki kuwa wasiwasi, kikubwa niseme tunafanya kazi kwa mujibu wa sheria na kanuni. Yeye ni Mwenyekiti wangu wa kamati ya ulinzi na usalama kwa hiyo ninaamini kama ana wasiwasi na chombo chake najua atakuja kutuita na kutuambia nini cha kufanya,” amesema Sirro.

“Lakini kama ana wasiwasi zaidi yeye ni kiongozi wetu atajua atachukua hatua gani dhidi yetu, kwa hiyo namuachia mkuu wangu wa kazi yeye ndio atajua nini cha kufanya.”
Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. ????????????????

    ReplyDelete
  2. kamanda una busara sana!!

    ReplyDelete
  3. Kam ni kweli waliokamatwa ni wengi na wako mikononi mwa vyombo vya usalama je ni kwanini wasifikishwe kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake?????? Ni kwa nini muruhusu hiyo hali ya kuumbuana mbele ya Waziri Mkuu juuu ya utendaji wenu wa kazi??????????? Mimi nadhani hapo kuna tatizo kubwa sana la kiuongozi na kiutawala; mawasiliano ni hafifu na utekelezaji wa shughuli zenu ni hafifu kabisaaaaaaa.......nadhani kuna mmoja wapo inabidi atumbuliwe kama sio Mkuu wa Mkoa basi awe huyo Kamanda Sirro. Na hiii itasaidia kuleta ufanisi wa shughuli za Kimkoa; Hayo malumbano ambayo yametokea mbele ya Waziri Mkuu ni dosari kubwa kwa utawala huu wa Awamu ya Tano.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad