VIDEO: ‘Nikikuta Mgambo Kituo cha Polisi Nitakula Sahani Moja na Sirro’-RC Makonda

November 21 2016 ziara ya mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda iliendelea katika jiji la Dar es salaam, katika ziara hiyo RC Makonda amekutana na wananchi wa Yombo Temeke ambao walitoa kero zao mbalimbali ikiwemo suala la usalama, migogoro ya ardhi, rushwa kwenye vituo vya polisi pamoja na kero za daladala kukatisha vituo.

Wakati akitoa ufafanuzi wa moja ya majibu ya kero, RC Makonda amesema jeshi la polisi limekuwa likichafuliwa na baadhi ya mgambo ambao wamekuwa wakiruhusiwa kufanya kazi kwenye vituo vya polisi hivyo amepiga marufuku mgambo hao kufanya kazi kwenye vituo vya polisi badala yake wawe kwenye ngazi ya mtaa.

’Ni marufuku kituo cha polisi kuwa na mgambo na mimi nitafanya operesheni zangu, nikikuta mkuu wa kituo ameacha mgambo kwenye kituo chake nitakula sahani moja na Kamishna Sirro, wakati mwingine Jeshi la polisi linapakwa matope kumbe ni matope ya mgambo’-RC Makonda

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad