DARASSA Awekwa Benchi na Madaktari Kutokana na Maumivu ya Kichwa


Rapa Darassa baada ya kunusurika kifo katika ajali mbaya ya gari akiwa na muongozaji wa video nchini Hanscana huko Kahama, Jamatano hii alienda katika hospitali ya Muhimbili jijini Dar es salaam kwaajili ya kucheki afya yake.

Darassa aliamua kwenda kucheki afya yake baada ya
kunusurika kifo kwenye ajali aliyopata jumapili iliyopita
.
.
. “Nipo hospitalini Muhimbili sasa hivi nawashukuru sana madaktari
wa hapa wamenipokea vizuri wamenipa huduma nzuri sana,” alisikika Darasa kupitia kipindi cha XXL cha Clouds FM
.
.
.
“Wamenicheki kwa sababu nilikuwa najisikia vibaya sana sehemu za kichwani nashukuru Mungu majibu yanaonyesha kila kitu kipo poa kabisa kuna damage ndogo wanaifanyia kazi naendelea na matibabu ila nimeshauriwa kupunguza mizunguko kwa wiki moja ili niweze kupumzika na kutibu hayo maumivu ya kichwa,” alisema Darasa
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad