DAVID Kafulila Ahama NCCR, Ahamia Chadema

Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Kusini kwa tiketi ya Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila leo ametangaza kukihama chama hicho na kusema kuwa atajiunga na Chama cha Demokrasia na Manendeleo (CHADEMA).

Kafulila ambaye alijizolea umaarufu mkubwa katika bunge la kumi kwa kufichua hoja mbalimbali za ufisadi amesema kuwa ameshawasilisha barua ya kujiuzulu kwa uongozi wa chama hicho.

Akieleza sababu iliyomsukuma kujiunga na CHADEMA, Kafulila alinukuliwa akisema kuwa kikubwa ni kuhakikia wanaleta mabadiliko nchini Tanzania.

"Ili kufanya safari kuwa fupi, kuondoa vikwazo vya huyu yuko chama hiki mwingine kile nimemamua kujiunga na CHADEMA ili kurahisisha uletaji mabadiliko katika nchi yetu sababu nimeona uhitaji huo," alisema Kafulila.

Katika uchaguzi uliopita Kafulila alipoteza jimbo la Kigoma Kusini ambalo lilikwenda wa Hasna Sudi Katunda Mwilima aliyekuwa akigombea kupitia Chama cha Mapinduzi.
Tags

Post a Comment

6 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Huyo ndio kwisha maneno yake. Zile dili za kihuni za kisiasa hakuna tena. Kwisha maneno yako.

    ReplyDelete
    Replies
    1. ANGALIA POVU LINAVYOKUTOKA!!! , ULITAKA HILO JEMBE LIENDE CHAMA CHA MAZINGAOMBWE AU ??,NA BADO MAPOVU KUWATOKA MJIANDAE!

      Delete
    2. mbona na wewe povu linakutoka??? chama cha mazingaombwe ni hicho unchokiamini wewe na unaonekana jinsi gani ulivyo juha kwa kutojitambua -mfyuuuuu

      Delete
  2. Hahahahahahahaha dah kwa kweeeeeliiiiiii HAPAKAZITU duh

    ReplyDelete
  3. Hana jipya, karuka 'matope' kayakanyaga 'mavi', hata Mbatia na wewe kwendraaaaaa.........HAPA KAZI TU

    ReplyDelete
  4. Spidi ya Magu inawahenyesha Vilaza

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad