KAULI ya Kocha wa Argentina Baada ya Maneno Kuzidi Kuwa Messi Anamchagulia Wachezaji

Moja kati ya vipindi vigumu kwa staa wa soka wa kimataifa wa Argentina anayeichezea FC Barcelona Lionel Messi ni kipindi hiki ambacho Argentina haifanyi vizuri sana, Lionel Messi ambaye ni nahodha wa Argentina aliwahi kulaumiwa na kuandikwa kuwa hajitumi timu ya taifa.

Lionel Messi pia amewahi kutuhumiwa kuwa amekuwa na sauti katika uchaguzi wa wachezaji wa timu ya taifa mbele ya kocha wao Edgardo Bauza madai ambayo kocha Bauza amekuwa akiyapuuzia na kukaa kimya.

Kocha Bauza ameamua kuzungumzia kuhusiana na maneno hayo “Kwa wale wanaofikiria kuwa Lionel Messi anachagua wachezaji wa kuunda kikosi cha timu ya taifa, sidhani kama kuna haja ya kuwajibu, kama Messi akichagua wachezaji basi nitakuwa nje ya timu”

Kama utakuwa unakumbuka October 14 Lionel Messi alidaiwa kuhusika na kuzuia mchezaji Mauro Icardi asiitwe timu ya taifa, kwa sababu alimchukua mke wa mchezaji mwenzake wa Argentina na rafiki yake ambaye amewahi kucheza nae FC Barcelona Maxi Lopez.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad