MC Pilipili: Nimerudi Darasani Kujinoa Kimombo ili Kujiandaa Kwenda Kimataifa

Mchekeshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias aka MC Pilipili amesema amerudi darasani kujinoa zaidi katika lugha ya Kiingereza, kama sehemu ya mikakati yake ya kwenda kimataifa.

Kwenye interview niliyofanya naye, Pilipili amesema japo Kiingereza ni lugha anayoielewa, angependa kuifanya iwe laini zaidi mdomoni mwake. Amesema tayari amemaliza kozi ya kwanza pale British Council na tayari ameshaona mabadiliko.

“Nimepiga pale miezi yangu mitatu, naanza mingine January halafu nitapiga module yangu ya tatu,” amesema.

“Nafanya hivyo kwasababu naamini kwamba once the student is ready, teacher will appear. Kwamba nitakapokuwa tayari kwaajili ya kimataifa, kwahiyo hata gigs za kimataifa zitaanza kutokea kwasababu unaanza kufanania.”


 VIDEO:TAZAMA MAAJABU YA KIJANA HUYU

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad