WAKILI Albert Msando Akatwa Katwa Mapanga Dar

Ndugu zangu, nawashukuruni wote mliojaribu kunitafuta na kunipa pole toka jana. Sikuwa napatikana kwa sababu walionivamia waliiba simu pamoja na vitu vingine.

Kilichotokea: Usiku wa saa tano siku ya Alhamisi (juzi) nilisimamishwa na gari baada kupigiwa honi na kuwashiwa taa na gari iliyokuwa nyuma yangu. Niliposhusha kioo driver akawa anaongea haraka haraka kwamba nimewagonga wakati narudi nyuma parking na nakimbia. Nikamjibu kwamba sijamgonga.

Akaniambia umetugonga angalia bampa. Kweli bampa lilikuwa limelegea. Ila sikuwa nimewagonga hivyo nikaendelea kubisha. Akaniambia shuka uangalie hata pembeni. Alikuwa amevaa smart tu so nikashuka. Wakati naangalia anaposema nimemgonga wakashuka wengine wawili kutoka kwenye gari na kunishika. Wakaanza kunishambulia huku wakinipora wallet, saa nk. Then wakanikata panga kichwani na kupekua gari wakaondoka na laptop na simu pamoja na funguo wa gari.

Kwa sasa naendelea vizuri baada ya kupata matibabu. Nawashukuru wote.

Albert Msando

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pole sana kaka mungu aendelee kukutetea

    ReplyDelete
  2. Pole sana,hii inafanana na yaliyonitokea wiki mbili zilizopita ila mimi chale zilinicheza,sikujali nini wanasema wala kushuka kwenye gari bali niliwaambia nifuateni nyuma twende polisi,na bila shaka hao umetoka nao mbali bila wewe kujua,wana mtandao wao.Ni aina mojawapo ya mbinu za uporaji,wao ndio wamelegeza bampa au wanagonga taa yako hata wanakugonga au kuvunja chochote ili mradi tu uingie kwenye mtego,na mara nyingi wanavizia sehemu ambayo watu hawako makini kwa tukio lolote,na ukishuka tu wanakushambulia,hivyo hata kama gari lako limegongwa achana nao,bora uende/ujipeleke polisi mwenyewe.

    ReplyDelete
  3. MWANDISHI UNATUSHTUA NA UDAKU WAKO,ANDIKA VIZURI.AMEKATWAKATWA AU AMEKATWA?

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad