YOUNG D 'Kwa Mara ya Kwanza Nimejisikia Tofauti Sana Baada ya Kumbeba tu Mwanangu'

Rapper Young Dee amesema kupata mtoto kumempa furaha ambayo hawajawahi kuwa nayo katika maisha yake.

Young amesema:

Kwa mara ya kwanza nimejisikia tofauti sana baada ya kumbeba tu mwanangu. Yaani nimejisikia tofauti hali ambayo sijawahi kuisikia wala kutegemea nitaisikia. Kwahiyo ni feeling mpya kabisa, yaani amenifanya nimepata kitu ambacho sijawahi kuwa nacho, nimepata kama nguvu hivi. Amenipa kila sababu ya kuamka asubuhi kwa kumfikiria yeye, chochote ambacho nakipata kinaenda kwa yeye. Yaani mpaka sasa hivi ameanza kubadilisha ratiba zangu, yaani kuna lifestyle ambayo naweza kuona ameshaweza kunibadilisha kwasababu kuna vitu ambavyo sivioni tena kuwa na umuhimu. Kuhusu uhusiano na mama yake ni uhusiano ambao uko vizuri sana sababu ni wa muda mrefu sijawahi kuacha kuwasiliana naye. Kwahiyo na hivi mtoto amezaliwa, nina uhakika utaimarika zaidi.

Mtoto wa Young Dee ni wa kike na anaitwa Tamar.
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hongera sana yound dee mtunze mwanao aje akutunze!!!!

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad