Aibu ya Mwaka Hii!! Amber Lulu Abambwa Akidendeka Live na Njemba Nnje ya Ukumbi,Tazama Picha Hapa +18..!!!

amber-lulu-5
DAR ES SALAAM: Video Queen mwenye vituko kila kukicha, Lulu Euggen ‘Amber Lulu’ Jumapili iliyopita alibambwa usiku wa manane  akifanya vitendo vichafu na msanii wa tamthiya ya Kelele aliyejulikana kwa jina moja la Talik, nje ya ukumbi wa Catalunya uliopo Mwenge Jijini Dar.

amber-lulu-6amber-lulu-1amber-lulu-7amber-lulu-8amber-lulu-4Video Queen huyo alikuwa ni mmoja wa waalikwa kwenye sherehe ya kuzaliwa staa wa Bongo Muvi Irene  Uwoya, ambapo baada ya kuingia na kupata ulabu kiasi cha kutosha, alitoka nje na kukaa pembeni ya gari akiwa na msanii huyo huku wakipigana mabusu mdomoni bila kujali wapita njia.

“Nyie huyu Lulu atakuwa amepagawa kabisa maana hata haogopi kabisa kama watu wanapita na kuwaona wanachofanya, na wakati huyu sasa hivi anajinadi yuko na Young D” alisikika kijana mmoja akizungumza.

Licha ya binti huyo kuhusishwa na Young D, zipo tetesi pia zinazomtaja msanii wa Hip Hop, Roma Mkatoliki kuwa pia anatoka naye kimahaba.

Mwandishi wa habari hii alimsogelea Lulu na kutaka kujua kulikoni kufanya mambo hayo hadharani, ambapo aligeuka mbogo na kutaka aachwe aendelee na mambo yake.“Dada yangu nakuheshimu, naomba uniache, tena uniache kabisa, hakuna aliyenilipia nauli ya kuja hapa hata mara moja,” alisema Lulu.Katika pati hiyo iliyohudhuriwa na mastaa kibao, waalikwa walikunywa na kula kwa muda wote kuanzia saa amber-lulu-3Wakijiachia kima-lovee.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Na hii ni habari ya zamani kwenye birthday ya Irene Owoya mnarudia tena aisee udaku hawana kumbu kumbu

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad