Kubwa Kuliko..!!! Shilole Awatolea Uvivu Wanaolia Njaa na Kumlalamikia Magufuli..!!!


Msanii wa muziki wa bongo fleva Zuhena Mohammed alimaarufu kama Shilole amefunguka na kuwapa neno baadhi ya vijana ambao wamekuwa wakilalamika juu ya hali ngumu ya maisha huku wengi wao wakiitupia lawama Serikali ya awamu ya tano.

Shilole kupitia mtandao wake wa Instgram amesema amewachana baadhi ya vijana hao na kusema wamekuwa wakilalamika kuwa kuna hali ngumu ya maisha au pesa haipatikani ikiwa wao wenyewe hawahitaji kujishughulisha wamebaki kukaa vijiweni pasipo kuhangaika kutafuta mishe za hapa na pale za kuingiza kipato.

“Unalalamika hali ngumu huku umekaa” aliandika Shilole  ambae yupo mikoa ya kanda ya ziwa akifanya shows.

Baadhi ya mashabiki wa Shilole wamemuunga mkono kutokana na kauli yake hiyo huku wengine pia wakionyesha kutokubaliana naye wakiendelea kusema kweli maisha ya sasa ni magumu na mishe hakuna.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. KWELI KABISA,VIJANA WENGI TULIZOEA NJIA HARAMU KUJIINGIZIA KIPATO NA NDIO WANAOLIA HALI NGUMU,SHILOLE ANAPIKA (MAMA NTILIE),ANAIMBA SAA NGAPI AKOSE HELA YA KULA?

    ReplyDelete
  2. Hahahahah mbona tumejifunza ujasiliamali bila kutegemea,nilizoea kutegemea posho za vikao na safari kama hela ya ziada kwenye mshahara wangu,imebidi nilime mbogamboga,nipike vitumbua,niwauzie wananchi.Ngosha akandamize tu,Tutazoe.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad