Kwa Wanaume Tu:Kwa Hizi Tabia, Huwezi Kujiita Mwanamme Mkamilifu Hata Siku Moja..!!!

Huwezi kujiita mwanamme kama hujui wanao wanakula nini?


Huwezi kujiita mwanamme kama hujui kama nguo walizovaa wanao pesa imetoka wapi?

Huwezi kujiita mwanamme kama hujui nguo aliyovaa mkeo, nywele alizosuka na kila kitu chake kimetoka wapi?

Mkeo kufanya kazi sio tiketi ya wewe kugeuka kuwa mwanamme suruali?

Kuna watu wengine hujisahau eti kisa mke anafanya kazi basi unafurahia kula kuku kila siku. Hata hujiongezi ukatoa matumizi ya ndani?

Ungekuwa na akili kidogo ungejua kuwa mshahara wa mkeo hautoshi kufanya vyote hivyo anavyofanya na ungekuwa makini, sasa wewe unaridhika tu kwakuwa anafanya kazi unamuachia kazi ya kuwa mwanamme.

Nikuambia tu kitu kimoja mwanamke hata awe na pesa vipi bado anahitaji mwanamme wa kumtunza, yaani mtu wa kwenda kumlalamikia shida zake na kumsikiliza. Sio kwenda kulalamikia shida zake kwenye ATM.

Katika familia mwanamme unatakiwa kutoa na mke kuchangia kwamba, hata kama ana kipato kikubwa lakini usibweteke na kumuachia kila kitu, asipoweza kulalamika kwako atatafuta sehemu ya kulalamikia.

Mwanamke anatakiwa kuongezea kilichopungua na si kutoa kisichokuepo.

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hayo maisha ni ya kizamaaaniiiii. Kwa sasa hivi zile Financial obligations ni equal. Hakuna cha mwanamke wala mwanaume. Ni lazima wote wawili wawajibike katika kuleta neema ndani ya nyumba yao. Ukiona mmojawapo anakuwa tegemezi kwa mwenzake kwa asilimia 100 ujue hapo hakuna kitu.

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad