Muda Wapita Tena Bila Jammeh Kuondoka Madarakani Gambia

Jammeh alikuwa ameomba apewe hadi saa 16:00 (saa moja jioni Afrika Mashariki) kufanya uamuzi kuhusu iwapo ataachia madaraka au la.

Makataa ya kwanza ya kumtaka aachie madaraka kufikia saa sita mchana yalikuwa yamepita.

Taarifa zinasema makamu wa rais wa zamani wa Gambia, Isatou Njie-Saidy, yupo ikulu ambapo anashiriki mazungumzo ya dakika za mwisho.

Marais wa Mauritania na Guinea wanajaribu kumshawishi Jammeh kuondoka.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad