Nay wa Mitego: MR T Touch bado ni producer mzuri lakini…


Nay wa Mitego na producer aliyemtambulisha kwenye game, Mr T Touch walikuwa na chemistry ya aina yake na walifanikiwa kutengeneza hits nyingi.

Baada ya kufanya kazi kwa muda katika studio za Free Nation za Nay, Touch aliamua kujiengua na kwenda kuanzisha studio yake mwenyewe. Huko bado anaendelea kufanya vizuri. Pamoja na kwamba hawafanyi tena kazi pamoja, Nay anakiri kuwa Touch bado ni producer mzuri.

“Ni producer mzuri, nimefanya naye kazi kwa muda mrefu so sidhani kama kutakuwa na kitu kipya cha ajabu toka kwake,” Nay alimuambia mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove.

Hata hivyo Nay anadai tangu aondoke Free Nation bado hajasikiliza ngoma mpya za producer huyo.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad