Obama amuonya Trump

Onyo la Obama kwa Trump

Rais mwendazake Barack Obama amuonya Donald Trump kutoendesha shughuli za white House kama 'Shughuli ya biashara ya familia '.

Donald Trump atarajiwa kuanza shughuli zake rasmi kama rais wa Maekani mnamo Januari 20.

Obama alikuwa anaongea kupitia runinga ya Marekani ya ABC news na kutoa wito kwa Trump kuheshimu taasisi za Marekani.

Alisisitiza kuwa Trump anafaa kuwa mwanaglifu kwa hatua atakazo chukua kwa kuwa atakuwa anaongoza kampuni kubwa zaidi duniani na nchi kubwa na yenye nguvu zaidi duniani.

Obama alikuwa wazi kusema kuwa Trump alisababisha mashambulizi ya mitandaoni yaliyotekelezwa na Uruusi.

Aidha Obama alimpendekezea Trump kuwa na imani na mashirika ya ujasusi ya taifa.

Hapo awali Donald Trump amepinga mashirika ya kufanya uchunguzi ya Marekani.

Kremlin hadi leo imekataa kuhusika na udukuzi wa mitandao ya Marekani.

Hata hivyo mashirika ya habari ka CNN,Washington Post na NBC yametangaza utambulisho wa majina ya watu waliohusika na udukuzi kutoka Urusi wakati wa uchaguzi wa Marekani.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. ??????????????????????????????????????????????????

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad