P-Funk Athibitisha Msichana Anayeonekana Kwenye Video Chafu iliyosambaa si Mwanae

Wiki iliyopita kulikuwa na tetesi kwenye mitandao ya kijamii kuwa mtoto wa Kajala aliyezaa na P-Funk, Paula ameonekana kwenye video chafu ya ngono.

Tetesi hizo zilidai kuwa kwenye video hiyo Paula anaonekana akifanya mapenzi na mwanaume ndani ya gari. Mama yake, Kajala alikanusha vikali kuwa anayeonekana si mwanae na kwamba tofauti na wengi wanavyodhani kuwa anamlea vibaya, amekuwa na msimamo mkali katika malezi yake.

Na sasa baba yake, Majani amezungumzia upande wake na kudai kuwa yeye pia ameiona video hiyo na kwamba msichana anayeonekana si Paula wake. Anadai kuwa atakuwa mzazi asiye na akili kushindwa kumtambua mwanae.

“Yule sio mtoto wetu amefanana naye labda kidogo tu,labda kiduku chake kile na nywele hivi,” Majani alikiambia kipindi cha Amplifaya cha Clouds FM.

Majani anadai kuwa kama Paula angehusishwa kwenye uchafu huo, pangechimbika. “Angekua mwanangu mnanijua mimi nilivyo,huyo mtu aliyeshoot hiyo video si kungekua na video yake na yeye labda anapewa kitu ushanielewa,” alisisitiza.

Majani alisema angemsaka mhusika, hata kama ni mtoto wa kizito na kumpeleka mbele ya sheria.

Mtayarishaji huyo mkongwe alisisitiza kile Kajala amewahi kusema kuwa, mtoto wa Paula hajawahi kuwa na simu na kwamba akaunti za Instagram zenye jina lake ni feki.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Pole sana watu washapasua,mla vya watu na vyake huliwa

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad