Producer Mr T Touchez Atoboa Siri ya Ngoma zake Kutamba Wakati Huu


Licha ya kufanya ngoma nyingi kali na kubwa mwaka 2016 Producer Mr T Touchez amefunguka na kusema kuwa bado hajafikia malengo yake kwani malengo yake kwenye muziki huu wa bongo fleva ni makubwa zaidi. .
.

Akiongea na EATV MR T Touchez amesema kipindi cha nyuma alikuwa anafanya ngoma kali na hits lakini kipindi hicho alikuwa bado hajalisoma game linataka nini na watu wanataka nini lakini sasa hivi ameshaweza kusoma watu wanapenda nini na game lipoje ndiyo maana kwake inakuwa rahisi sana kutengeneza hits song na kubadili muziki wake awezavyo na bado akaendelea kutoa ngoma kali tu.
.
. "Mwanzo nilikuwa nafanya muziki lakini nilikuwa silisomi 'game' japo nilikuwa naweza kutengeneza hits nyingi lakini si kama ilivyo sasa naweza kusema nataka kutengeneza hits song, au nataka kutengeneza idea ya muziki flani na nikaipeleka ikatiki kutokana na mimi kuisoma vizuri game na kuwa na juhudi zaidi katika kazi nazofanya kwa sababu nilikuja kugundua sijawa mkubwa kama vile mimi nataka kuwa, mpaka saizi bado sijakuwa vile mimi nataka sababu nina malengo makubwa tofauti na haya watu wanayaona" alisema @mrttouchez
#letitshine
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad