Rais Mstaafu Wa Ureno Afariki Dunia

Rais wa zamani wa nchi ya Ureno, Mario Soares ambaye anaheshimika kama baba wa demokrasia nchini humo amefariki dunia hapo jana akiwa na umri wa miaka 92.

Rais huyo wa zamani ndiye mwanzilishi wa chama cha kisoshalisiti nchini humo na katika kipindi cha uhai wake alitumia miongo kadhaa katika masuala ya siasa ikiwa ni pamoja na kuwa mstari wa mbele wakati wa mchakato wa nchi hiyo kujiunga kwenye Umoja wa Ulaya.

Soares alikuwa rais wa nchi hiyo katika kipindi cha kuanzia mwaka 1986 hadi mwaka 1996 baada ya kuwa tayari amelitumikia taifa hilo katika nyadhifa za uwaziri wa mambo ya nchi za nje na Waziri Mkuu.

Ureno imetangaza siku tatu za maombolezo kuanzia Jumatatu kwa ajili ya kuomboleza kifo cha kiongozi huyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad