Web

‘Shishi Food’ ya Shilole Yatoa Deal Kwa Wasichana

Top Post Ad


Msanii wa muziki Shilole kupitia kampuni yake ya mapishi ‘Shishi Food’ ametoa deal kwa wasichana wenye uwezo wa kupika pamoja na kutoa huduma.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Mtoto Mdogo’ yupo kwenye mpango wa kufungua mgahawa mkubwa maeneo ya Kinondoni jijini Dar es salaam.

Jumatano hii ametoa tangazo rasmi la kuhitaji wafanyakazi kwa ajili ya mgahawa huyo.

“Shishi Food delivery’ inatangaza nafasi ya kazi kwa wasichana tu. Kama unaujuzi wa chakula, na upishi pamoja na huduma kwa mteja.. tafadhari tuma picha pamoja na CV yako suzilitasamson@gmail.com,” aliandika muimbaji huyo Instagram.

Muimbaji huyo alikuwa na mgahawa Mwananyama Kinondoni lakini baadaye ukafungwa.

Below Post Ad

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Nafuu kalitoa lile jina la Shishi Trump

    ReplyDelete