Simu Yaweza Kumuingiza Matatizoni Paul Pogba


 Kiungo wa bei kubwa wa Manchester United, Paul Pogba anaweza kuingia matatani baada ya kuonekana akiendesha gari huku akitumia simu kitu ambacho ni kinyume na sheria za uendeshaji gari nchini England.

Pogba ameonekana akiendesha gari lake aina ya ua Audi RS6-R lenye thamani ya pauni 85,000 alipokuwa akiwasili mazoezini kwenye Uwanja wa Carrington, Ijumaa iliyopita.

Picha zimemuonyesha akiwa ameishika simu yake hiyo huku akiendesha gari na kama mamlaka husika za usalama barabarani zitaamua kutumia picha hiyo zinaweza kumuingiza matatizoni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad