U Heard: Camera ilivyosababisha Beef kati ya Q Chilla na MB Dog

Jana January 11 2016 kwenye U Heard ya Clouds FM kuna taarifa kutoka kwa Soudy Brown kama wewe ni mpenzi wa stori zote za Entertaiment nisingependa upitwe na hii ya kinachoelezwa kuwa ni beef kati ya wasanii Qchilla na MB Dog kutoka kwenye kampuni ya QS Muhonda.

Chanzo cha beef zinaripotiwa kuwa ni upotevu wa Camera ambayo taarifa za mwanzo zinasema kuwa Q Chilla ni muhusika kwenye wizi huo, baada ya Soudy Brown kumtafuta Q Chilla na haya ndiyo yalikuwa majibu yake kutokana na wizi huo wa Camera.

‘Mimi nakaa na wadogo zangu pale nyumbani na hawana tabia ya udokozi ila najua kuna watu wamewekwa kwa ajili ya kunifuatilia na unajua matatizo mimi na MB Dog yalianza kuanzia wake zetu, kwa sababu mimi na Mb Dog tunakaa Apartment moja na haya ni makosa ya QS kutuweka wasanii sehemu moja’ kuhusu camera sisi hatuna shida na camera‘>>>Q Chilla
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad