Ubuyu wa Moto Moto..Simu yawagombanisha Vanessa na Jux..!!!


Msanii wa muziki wa bongo fleva Vanessa Mdee amefunguka na kuweka wazi kuwa mara nyingi huwa wanagombana na mpenzi wake huyo Jux kutokana na tabia yake ya kuchelewa kujibu jumbe fupi au hata kupokea simu zake. 

Vanessa Mdee alisema haya kwenye kipindi cha 'Ngaz kwa Ngaz' kinachorushwa na ting'a namba moja kwa vijana EATV na kudai kuwa Jux kwenye suala la simu amekuwa mvivu sana na ndiyo jambo linaloleta tofauti kati yao.

"Mvivu wa simu amefarakanishwa na simu yake huyu jamaa, hata kwenye kujibu txt au kupokea simu hana ushirikiano na simu kabisaa kwa hiyo tunagombanaga mara nyingi kuhusiana na communication" alisema Vanessa Mdee 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad