Utafiti: Watu 550,000 waathirika na matumizi ya dawa za kulevya nchini

Tatizo la matumizi ya dawa za kulevya nchini ni kubwa ambapo utafiti uliofanywa mwaka 2014 unaonyesha kuwa watu elfu hamsini wameathirika kwa kutumia njia ya kujidunga sindano na watu laki tano kwa njia ya uvutaji.


Daktari bingwa wa magonjwa ya afya ya akili wa hospitali ya taifa Muhimbili Dk Kassian Nyandindi amesema utafiti uliofanywa mwaka 2014 umebaini na idadi hiyo ni kwa wale wanaotumia dawa aina ya heroin na cocaine lakini kuna wengine ambao hupatiwa huduma katika kliniki zao wanaotumia bangi,mirungi na pombe.

Aidha Dk Nyandindi amesema ingawa idadi ya watu walioathiriwa na dawa za kulevya nchini kwa sasa ni 25,000 waliojitokeza kupatiwa huduma katika kliniki nne zinazotoa huduma hiyo ni 3,500 tu na kuongeza kuwa kiwango cha HIV kwa kundi hilo ni asilimia 20 hadi 50 huku akitaja changamoto zinazoikabili idara hiyo.

Source: ITV

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. the goverment should not take the reality to be the source of solution... kabla kuweka majasusi wengi kukabiliana na unga muhimu ni kujua kwanini vijana wengi wameathirika na unga and vipi this can be turned around.. rushwa kwa walinzi wakorofi ndio unga unapita best solution ni kuhakikisha hakuna market for that shit.... tanzania invest in the youth...

    ReplyDelete
  2. Hiyo idadi si sawa labda sababu wengi wanatumia madawa kwa siri wanajificha ni kama ukimwi wengi wanao lakini hawajijui na wengi hawajapima huwa mnachukulia idadi ya wale waliopima tu

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad