Waganda Kuamua Mechi za Watanzania Kimataifa


Waamuzi wa Uganda wameteuliwa kusimamia mapambano ya raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika inayoanza Mwezi Februari mwaka huu.

Kamati ya waamuzi ya CAF, imewateua, Mashood Ssali, Hussein Bugembe, Musa Balikoowa Ngobi na Ali Sabila Chelegat kwa ajili ya mchezo wa Zimamoto dhidi ya Ferroviara da Beira, ya Msumbiji, utakaopigwa Februari pili mwa huu, 2017.

Kwa upande wa Tanzania Bara, Alex Muhambi, Ronald Katenya, Okello Lee na Brian Miiro Nsubuga wameteuliwa kusimamia mchezo wa Yanga dhidi ya Ngaya Club De Mde, ya Comoro, wikiend ya Februari 17 -19, 2017.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad