WASANII Wetu na Mtego wa Tuzo za Kimataifa

Naomba wakati tunakaribisha mwaka mpya 2017 tujadili kidogo hizi tuzo za kimataifa. Kwa sasa kumekuwa na wimbi la wasanii wetu kuwa nominated kwenye tuzo za nchi za wenzetu katika hii miaka miwili iliyopita.

Tumeona wasanii wetu wa muziki, movie na ata wanamitindo wakiwania tuzo na wengine kupata hizo tuzo ambazo tunaziita za kimataifa.

Mimi concern yangu ni moja tu. Hivi hizi tuzo mbona tumekuwa tunazipata kirahisi sana siku hizi.

Ukawii kusikia Harmonize ni msanii bora anaechipukia ndani ya Africa yote, au Wema Sepetu ni muigizaji bora east africa kwenye tuzo huko Uganda.

Hivi hizi tuzo uwa tunastahili au kwa kuwa zinaitaji wapiga kula ndio maana tunazibeba kirahisi?

Awa watu wanaotupa hizi tuzo kirahisi Hivi ni sababu wanaukubali muziki wetu au wanafanya kutafuta kufahamika na kutanua tuzo zao mpaka huku East Africa na wanaona Tanzania kwenye entertainment tupo vizuri hivyo ni kama wananatutumia kufanya biashara!?

Hivi mnaamini kuna msanii toka Tanzania amefanya vizuri mwaka huu kuliko Wizkid na Techno? Kama kuna wanaofanya vizuri kuliko awa mbona hatuwaoni wakipata mialiko ya kutumbuiza kama awa wanaijeria tunaochukua tuzo mbele yao? Mbona hatuoni muziki wetu ukipata rotation ya kutosha kwenye stations za radio na tv za nchi za wenzetu?

Hizi tuzo zinapeleka mbele muziki wetu au zinatudumaza? Maana tusije kudhani muziki wetu unakuwa sababu tunapata tuzo kirahisi kumbe zinatupumbaza!

Mimi binafsi naamini sana tuzo za Mama mtv na BET maana zinatoa atleast watu wanaoeleweka ila hizi tuzo zingine siziamni kabisa sijui kwa nini.

Naona sasa hivi mpaka kina Martin Kadinda nao wanapata tuzo za kudesign.

Okay ebu kama kuna mtu ana maoni tuweze kushare kuhusu huu utitiri wa tuzo.

By Gado/JF
Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. We mjinga nn sasa wasipate tuzo kwann kwan kazi zao si zinawawakilisha acha roho mbaya ww martin kadinda asipate kwann...ndo maana huendelei sababu ya negativity kwenye kila kitu....

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad