Video.Mbwana Samatta Azidi Kuwakuna Wazungu kwa Kiwango kikubwa cha Kufumania Nyavu..!!


Nahodha wa timu a taifa ya Tanzania , Mbwana Samatta amezidi kuwasha moto katika ligi kuu ya Ubelgiji maarufu kama Jupiler Pro League baada ya kuifungia timu yake ya KRC Genk bao moja katika ushindi wa mabao 3-0 walioupata wakiwa ugenini usiku wa Ijumaa hii dhidi ya Sint-Truiden.

Mabao ya Genk yalifungwa na Alejandro Pozuelo Melero dakika ya 37, Mbwana Ally Samatta dakika ya 39 na Ruslan Malinovskiy dakika ya 45.

Kwa sasa Genk wanashika nafasi ya tano katika ligi hiyo wakiwa na pointi 41 huku klabu ya Club Brugge ndio wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 52.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad