Askofu Mokiwa Aaibnishwa Mbele ya Kanisa,Waraka wa Makosa Yake Wasambazwa Kila Usharika..!!!


Waraka wa Askofu Mkuu wa Anglikana nchini, Jacob Chimeledya umesomwa katika makanisa yote ya Dayosisi ya Dar es Salaam ukibainisha makosa yaliyofanywa na Askofu Valentino Mkokiwa na kumtaka kujiuzulu wadhifa wake.

Waraka huo umesomwa kanisa la Mtakatifu Albano leo na mjumbe wa halmashauri ya walei dayosisi hiyo, Helen Mkoma umebainisha kwamba Januari 28 mwaka huu, Askofu Chimeledya aliunda kamati ya kwenda kuzungumza na Askofu Mokiwa wakimtaka ajiuzulu kwa hiari ili kulinusuru kanisa hilo.

Hata hivyo, Askofu Mokiwa aliomba muda wa wiki mbili ili kutafakari suala hilo lakini wiki mbili zimekwisha hajatoa mrejesho wowote huku kukiwa na viashiria vya kwamba hayuko tayari kutii agizo hilo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad