Imefichuka... Unene Kupita Kiasi Chanzo cha Ugonjwa wa Kansa..!!!


WANASAYANSI wa Uingereza wanasema wamethibitisha kuwepo kwa uhusiano mkubwa kati ya kunenepa na aina 11 za saratani.

Watafiti wamebaini unene unasababisha saratani kadhaa ikiwemo saratani ya tumbo, ini, matiti, utumbo na mfuko wa kizazi.

Watafiti hao kutoka Chuo Kikuu cha Imperial jijini London, wanasema, mbali ya kuepuka uvutaji sigara, kutunza uzani unaozingatia afya bora, ni njia muhimu inayopunguza uwezekano wa kuugua saratani.

Shirika la afya duniani linasema asilimia 40 ya watu wazima kote duniani ni wanene.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad