Kesi ya Masogange Yafikia Hatua Hii...!!!!!


 Upelelezi wa kesi ya kutumia dawa za kulevya inayomkabili  Agnes Gerald Waya maarufu kama Masogange(28) katika Mahakama ya Kisutu bado haujakamilika.

Wakili wa Serikali, Adolf Mkini ameeleza hayo leo wakati kesi ilipotajwa kwa Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbroad Mashauri.

Mkini alidai kuwa upelelezi bado haujakamilika na mshtakiwa hayupo mahakamani hapo.

Baada ya kueleza hayo, wakili wa Masogange, Nictogen Itege ameiambia Mahakama kuwa mteja wako hiyo alikuwa njiani kuelekea mahakamani lakini alikwama katika foleni eneo la Jangwani.

Masogange anakabiliwa na mashtaka mawili ya kutumia dawa za kulevya aina ya Heroin na Oxazepam.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad