Kimenukaaa...Magufuli Aanza Tumbua Tumbua Tena..Amtumbua Katibu Mkuu wa Wizara...!!!!!


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi na kumsimamisha kazi Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge) Bw. Uledi Abbas Mussa.

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa kutenguliwa kwa uteuzi na kusimamishwa kazi kwa Bw. Uledi Abbas Mussa kunaanzia leo tarehe 15 Machi, 2017.

Hatua hiyo imechukuliwa ili kupisha uchunguzi zaidi dhidi ya Bw. Uledi Abbas Mussa kufuatia kutozingatiwa kwa taratibu zinazotakiwa katika kushughulikia masuala ya uwekezaji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad