Kimenukaaa...Wema Sepetu Mbioni Kukumbwa na Hukumu Kali na Ya Kihistoria...!!!


Upelelezi wa kesi ya kukutwa na bangi inayomkabili Msanii maarufu nchini wa fani ya uigizaji wa filamu, Wema  Sepetu (28) na wenzake wawili akiwemo mfanyakazi wake wa ndani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu upo katika hatua za mwisho kukamilika.

Wakili wa Serikali Constantine Kakula ameeleza hayo jana (Jumatano) mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati kesi hiyo ilipotajwa.

Baada ya kutolewa kwa maelezo hayo, Hakimu Simba aliuhimiza upande wa mashtaka wajitahidi kuukamilisha na kesi imeahirishwa hadi Aprili 11 ,2017. 

Mbali na Wema wengine wanaokabiliwa na kesi hiyo ni mfanyakazi wake wa ndani, Angelina Msigwa (21) na Matrida Seleman Abbas (16) aliyetambuliwa kuwa ni mkulima wote wanatetewa na wakili Hekima Mwesigwa.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad