Magufuli Awapa Makavu Live Walioimba Wanaimani na Lowassa Mbele ya Kikwete..!!!


Mwenyekiti wa Taifa CCM, Rais John Magufuli amewataka
makatibu wa mikoa wa chama hicho wanaotaka kuingia katika vikao vya
Halmashauri Kuu  (Nec) ya Taifa ya chama hicho wakagombee uenyekiti.

Akizungumza jana (Jumamosi) wakati wa ufunguzi wa kikao cha Nec, Rais Magufuli amesema
kuna watu wanaumuhimu wa kuingia katika vikao vya Halmashauri Kuu na
kwamba wakikosa kutakosekana uwakilishi .

“Nikawaambia mbona mwaka uliopita waliposimama wakimpinga mwenyekiti
makatibu mlikuwepo? Wakati mwenyekiti anawalipa mshahara mbona
hamkumtetea? Mbona hamkusimama kupigana na bado wakaendelea  kuimba
wanaimani na mtu fulani na wengine mkawa mnaitikia,”amesema.

Amesema kwa kuwa mabadiliko ya Katiba na Kanuni ambayo yatapunguza
idadi ya wajumbe wa vikao vya juu vya chama hicho walishayajadili
katika  kikao kilichofanyika Desemba 13 mwaka jana, ni matumaini yake
kuwa kikao hicho hakitachukua muda mrefu kuyajadili.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad