Makonda Afunguka Mapya Vita Dawa za Kulevya...!!!


MKUU  wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amesema kelele zinazoendelea dhidi yake ni dalili za mafanikio katika vita dhidi ya dawa za kulevya.

Makonda ameyasema hayo jana alipokuwa mgeni rasmi katika tamasha la Twendezetu Kigamboni lililofanyika Kigamboni jijini Dar es Salaam ambako alisisitiza kwamba mapambano dhidi ya dawa za kulevya ni vita vya ya kufa au kupona.

“Mfahamu kuwa tunapambana kati ya mauti na uzima, kelele na mwangwi unaoendelea sasa ni dalili njema kwamba tunaendelea kunyooka,” amesema Makonda.

Makonda alisema Dar es Salaam ya sasa anaifananisha na chuma kilichopinda na sasa kiko katika hatua ya kunyooka hivyo lazima zitokee kelele nyingi kama ambavyo zinaendelea sasa.

“Huwezi kufanya kazi ya kunyoosha chuma bila kusikia mwangi, kelele na maumivu kwa sababu kazi ya kukomboa vijana dhidi ya dawa za kulevya si rahisi,” alisema Makonda.

Tamasha hilo lilihudhuriwa na vingozi wengine wa serikali akiwemo  Mbunge wa Jimbo hilo, Dk Faustine Ndungulile, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Rahel Mhando na Katibu Tawala wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo.

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Ni nani aliyeipindisha nchi hii kama siyo utawala wa miska kumi chini ya CCM. Na kama siyo chini ya kiongoziKikwete ambaye anamajina ya wahusika wakuu. Je kama si CCM inayopindisha na kufunika ukweli ni nani? Tumembadili tu kiongozi lakini ni CCM iliyutawsla nyuma. Sijasikia CCM kuifanyia kazi orodha ya Kikwete je kwa nini

    ReplyDelete

Top Post Ad

Below Post Ad